Thursday, 28 November 2013

[AUDIO] MSIKILIZE HAPA MADAM RITA AJIBU MASWALI TISA MUHIMU KUHUSU EBSS 2013 ....!


Shindano la EBSS 2013 linaelekea ukingoni ambapo
November 30, atatangazwa mshindi wa shindano hilo pale
Escape 1, Dar es Salaam.
Washiriki watano waliobaki katika shindano hilo ni
Emmanuel Msuya, Elizabeth Mwakijambile, Amina Chibaba,
Melisa John na Maina Thadei.
Times Fm imefanya mahojiano na Chief Judge wa shindano
hilo, Rita Paulsen aka Madam Rita, na ameweza kujibu
vizuri maswali tisa muhimu.
Watu wengi hawakutegemea Mandela angeondolewa kati ya
washiriki sita, na walitegemea awe kati ya watano, ni upi
mtazamo wako kwa kuzingatia kuwa ulionesha kumkubali
sana?
Mandela pale alipofikia wamemshinda wenzake, lakini sio
kwamba sio muimbaji mzuri. Tunahitaji mshindi mmoja,
kwa hiyo ubora umezidiana na nafikiri hata watazamaji
wanakubalina kwamba hapo alipokuwa amefikia wenzake
ambao wamebaki wanamzidi hata ukiwaweka kwa pamoja,
I’m sure.
Kwa hiyo, ndio kuna mashabiki lakini mshindi lazima awe
na uwezo wa kuimba sio tu mshindi kwa sababu watu
wanashabikia. Lakini sio kwamba hawezi, huwezi kuwa
kama huwezi halafu ukafika top ten, Mandela amefika hadi
top six.
Kuna wasichana wanne na mvulana mmoja tu kati ya
washiriki walioingia fainali, je hii inaonesha kuwa
wasichana wanauwezo zaidi?
Imetokea, sisi huwa tunaangalia vipaji zaidi kuliko gender,
imetokea kwamba wasichana wamefanya vizuri kuliko
wanaume this year. Kwa hiyo kitu ambacho kimetokea na
sio kwamba imepangwa au nini…Imetokea kwamba this
year wasichana wamekaza buti na wamefanya vizuri
mpaka wakafikia top 4.
Kuna wakati nyie kama Majaji huwa mnatofautiana na
unaonesha kukasirika, je huwa iko serious?
yeah..Huwa inakuwa serious, yeah ni serious!
Unazungumziaje comments za Salama kwa kuwa mara
nyingi amekua ‘akimchana’ mshiriki, halafu unaoneka
haufarahii alichokisema na hata unabadilika emotionally?
Mimi sina tatizo nae na na-react kutokana na ninavyokuwa
najisikia. Lakini Salama mimi namkubali kwa sababu
analeta changamoto kwa washiriki na analeta changamoto
kwenye meza ya Majaji na ndio maana yupo leo mwaka wa
saba. Sina tatizo nayo kwa sababu otherwise itakuwa
boring inabidi kuwepo na changamoto. Yeye anaujasiri wa
kuweza kuongea anavyoongea na mimi naweza kuongea
ninavyoongea.
Niseme tu kwamba kila Jaji ambaye yuko kwenye ile meza
ni real, hakuna mtu anafake au whatever. Kila mtu
anakuwa anaongea hisia zake zinavyomtuma.
Ukizingatia hii ni reality show na kuna washiriki wanataka
kusikia yeye anasema nini na hawajali mimi nasema nini,
na kuna watazamaji wanataka kusikia yeye anasema nini
na wala hawataki kusikia mimi nasema nini. Na hiyo ndio
imeifanya EBSS kuwa EBSS…Entertainment.
Kwa kuwa washiriki wote wamekaa nyumba moja kama
familia, je huwa wanagombana? Na kama ndiyo, ni njia gani
inatumika kuhakikisha wanaenda sawa?
Of course wanagombana, kuna uongozi kuna sheria ambao
wanakuwa wanafuatilia, kuna walimu na kuna watu
wanaowakosoa. Kwa hiyo it’s a proper organized thing,
kuna uongozi kabisa kwenye EBSS. Na ikitokea nisema nao
natokea, kwa hiyo kuna discipline ya hali ya juu na
discipliners wapo pia.
Ni mshiriki yupi ambaye wewe unaweza kumtaja kama
mshiriki mwenye nidhamu/mtiifu zaidi?
Kusema ukweli wote walioshiriki mwaka huu ni watiifu na
wana tabia nzuri, they are good kids nashukuru Mungu.
Hatujawa na matatizo ya watu kukosa nidhamu, ni vijana
wazuri na wasikivu na hakuna hata mmoja wao mwenye
tatizo
Ni mshiriki gani ‘mmoja’ aliyetoka katika shindano hilo
lakini kutokana na uwezo wake ungependa sana angekuwa
kati ya hawa watano?
Mandela, Mandela..! Tutaangalia pia jinsi ya kumsaidia
kama muigizaji (Benchmark Production), I think ni
muigizaji zaidi kuliko muimbaji.
Ni ipi picha halisi ya show ijayo ya fainali ya EBSS 2013 na
maandalizi, kwa kuzingatia kuwa siku hizi watu huangalia
zaidi ubora wa show?
Ni changamoto, lakini mimi naweza kuzungumza kuwa
itakuwa very nice, itakua nzuri sana kutokana na..sisi
tunapenda kubadilisha na kuwa na vitu vipya kila mwaka.
Na mwaka huu hiyo ni changamoto kwetu, hiyo ni sehemu
mpya kwetu ni venue mpya pale Escape 1, lakini itakuwa
bomba kinoma.
Watu wengi wanatamani P-Funk Majani arudi kwenye meza
ya Majaji, wewe kama Chief Judge unalichukuliaje?
Hili tutalifanyia kazi!
by timesfmradio
Times Q&A, Madame Rita akiongea na www.timesfm.co.tz
07:05
97 0 0 0 Share Like
Share

No comments:

Post a Comment