TIMU ya taifa ya Uruguay imefanikiwa kutinga hatua ya 16 bora ya Kombe la Dunia nchini Brazil, lakini kituko ni straika wa timu hiyo, Luis Suarez kumng’ata beki wa Italia kwenye Dimba la Das Dunas.
Uruguay imefuzu hatua hiyo baada ya
kuifunga Italia bao 1-0 katika mechi ya mwisho ya Kundi D ikiungana na
Costa Rica ambayo ilitoka suluhu ya 0-0 dhidi ya England katika mechi ya
mwisho pia kwenye Uwanja wa Mineirão.
Bao pekee lilifungwa kwa kichwa katika dakika ya 81 na Diego Godin ambaye ndiye nahodha, kutokana na mpira wa kona.
Mara baada ya kung’atwa, Darmian alilalamika kwa mwamuzi huku akimuonyesha bega lake lakini hakuna uamuzi wowote uliochukuliwa.
Katika mechi ya England ambayo
ilikuwa ikikamilisha ratiba, ilitumia wachezaji wengi ambao hawakuwemo
kwenye mechi mbili za awali, ilishindwa kupata ushindi hiyo, kumaliza
michuano ikiwa na pointi moja.
No comments:
Post a Comment