Wednesday, 18 June 2014

STAA WASTARA APINGA MASTAA KUAGWA LEADERS.sababu ijue hapa!

STAA WASTARA APINGA MASTAA KUAGWA LEADERS.sababu ijue hapa!


Wastara Juma akiwa katika moja ya msiba wa wasanii wa Bongo Muvi .

Mkali wa sinema za Kibongo, Wastara Juma amepinga kitendo cha mastaa wa Bongo kuagwa Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar wanapokutwa na umauti.

Mkali wa sinema za Kibongo, Wastara Juma.
Akizungumza na paparazi juzikati, Wastara alieleza kwa huzuni kubwa kuwa hafurahii eneo la Leaders kutumika kuagia kwa sababu ni eneo hilohilo ambalo hutumiwa kwa starehe.

“Ukweli kwa upande wangu napinga mastaa kuagwa Leaders kwa sababu Leaders mara nyingi hutumika kama sehemu ya anasa. “Ningeiomba serikali itutafutie sehemu maalum kwa ajili ya kufanyia shughuli zote za misiba ya watu maarufu,” alisema Wastara.

No comments:

Post a Comment