Askari polisi wa kituo kikuu
cha Polisi cha kati akiwa amemshikilia kijana mmoja baada ya kumuokoa
toka mikononi mwa madereva bodaboda ambao walikwishaanza kujichukulia
sheria mkononi kwa kumuadhibu baada ya kutaka kuiba pikipiki.
Askari
katika ofisi ya kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro walilazimika
kufunga geti kuzuia kundi kubwa la madereva boda boda na watu wengine
wakilazimisha kuingia ili kumfuata mwizi wao wa pikipiki.
Madereva hao walionekana kukerwa na kuzuiwa kumuadhibu kijana huyo na hapa walionekana wakilalamika.
Jamaa wa nje akatamani kupita katikati ya Nondo hapa.
Geti likafungwa na hakuna mtu aliyepita.
No comments:
Post a Comment