Sunday, 1 June 2014

BREAKING NEWS: MASKINI! MTOTO ALIYEWEKWA KWENYE BOKSI MIAKA 4 AFARIKI



BREAKING NEWS: MASKINI! MTOTO ALIYEWEKWA KWENYE BOKSI MIAKA 4 AFARIKI

Nasrah Rashid (kulia) enzi za uhai wake. Kushoto aliyekaa ni baba yake mzazi Rashid Mvungi.


Baba wa mtoto Nasrah, Rashid
Mvungi (47) akiingizwa mahabusu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi
Morogoro baada ya kupandishwa kizimbani kujibu mashitaka ya kula njama
na kufanya ukatili dhidi ya mtoto Nasra.
Nasrah Rashid enzi za uhai wake.
Watuhumiwa wengine kwenye sakata hilo mama mlezi, Mariam Said (38) wa kwanza kushoto na mume wake Mtonga Omar (30) wa kwanza kulia wakisindikizwa mahabusu chini ya ulinzi wa polisi baada ya kusomewa mashitaka.
MTOTO
Nasrah Rashid (4) aliyekuwa akitibiwa katika Hospitali ya Taifa
Muhimbili baada ya kuugua na kupata ulemavu kwa kufungiwa kwenye boksi
miaka minne amefariki dunia.




 Nasrah
alifichwa kwenye boksi na mama yake mkubwa aitwaye Mariamu Said mkazi
wa Kiwanja cha Ndege, Morogoro tangu akiwa na miezi tisa baada ya mama
yake mzazi kufariki. 




Tunalaani
vitendo hivi vya kikatili alichofanyiwa mtoto huyo licha ya madaktari
kujitahidi kuokoa maisha yake lakini mungu ameamua kumchukua....




MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI. AMEN!

No comments:

Post a Comment