Friday, 6 June 2014

BABY MADAHA AFUNGUKA, "SIAMINI KAMA ADAM KUAMBIANA NA RECHO WAMEKUFA MPAKA NIONE MAKABURI"

BABY MADAHA AFUNGUKA, "SIAMINI KAMA ADAM KUAMBIANA NA RECHO WAMEKUFA MPAKA NIONE MAKABURI"

MSANII wa filamu na muziki Bongo, Baby Joseph Madaha (pichani juu) ambaye kwa sasa yuko Kenya amesema kuwa, haamini kama kweli wasanii wa filamu Recho Haule na Adam Kuambiana wamefariki dunia mpaka siku atakapoyaona makaburi yao.

Maziko ya Msanii Recho yaliyofanyika katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar.

Akizungumza na Ijumaa kwa njia ya simu, Madaha alisema ameshitushwa na vifo hivyo na vimemfanya akose amani kutokana na namna walivyoondoka duniani ghafla.
 Jeneza lenye mwili wa marehemu Adam Kuambiana.

“Nilitamani sana kuwepo lakini niko mpakani mwa Kenya na Uganda kuna ziara maalum ya kikazi naifanya.
Yaani bado siamini kama kweli wamefariki, mpaka nije nione walipozikwa,” alisema Baby Madaha.

No comments:

Post a Comment