Wednesday, 28 May 2014

MASTAA WAONESHANA JEURI YA FEDHA KWENYE HARUSI



MASTAA WAONESHANA JEURI YA FEDHA KWENYE HARUSI



FEDHA inaongea!
Mastaa wanaowakilisha Klabu ya Bongo Movie Unity na Shirikisho la
Filamu Nchini (TAFF) wameonesha jeuri ya fedha kwa kuwatunza maharusi,
mwigizaji Vanita Omary na mumewe Paul Mtenda.




Mastaa wa Bongo Movies wakionyesha jeuri ya fedha katika harusi ya msanii Vanita Omary na mumewe Paul Mtenda.
Sherehe
hiyo ilifanyika Jumamosi iliyopita katika Ukumbi wa Mwika, Sinza jijini
Dar ambapo pamoja na zawadi nyingine, maharusi hao waliondoka na
shilingi millioni tatu, fedha taslimu.
Mpango
mzima wa kuwamwaga ‘minoti’ uliongozwa na muigizaji Yobnesh Yusuf
‘Batuli’, Mwenyekiti wa Bongo Movie, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’,
Jacob Steven ‘JB’, Kulwa Kikumba ‘Dude’ na wengineo ambapo mwishoni
hesabu ya jumla ilitimia shilingi milioni tatu.
Mwenyekiti wa Bongo Movies, Steve Nyerere akisherehesha katika harusi hiyo.
Kwenye
sherehe hiyo, hawakuonesha utengano, hawakujali kama ni memba wa Bongo
Movie au Shirikisho la Filamu Nchini (TAFF) lililowakilishwa na rais
wake, Simon Mwakifamba ambaye muda wote alionekana mwenye furaha.
Paul Mtenda akiwa na 'mai waifu wake' Vanitha.
Mbali
na Steve Nyerere, JB, Batuli na Dude, mastaa wengine waliohudhuria
sherehe hiyo ni pamoja na Issa Mussa ’Cloud 112’, Elizabeth Michael
‘Lulu’, William Mtitu, Single Mtambalike ‘Rich’, Yvonney Cherry
‘Monalisa’, Suzan Lewis ‘Natasha’ na wengine wengi.


No comments:

Post a Comment