Siti, binti wa Mbunge wa Temeke Abbas Mtemvu, usiku wa kuamkia jana ameibuka kidedea katika kinyang’anyiro cha kumsaka mrembo wa Tanzania (Redd’s Miss Tanzania 2014) katika shindano lililofanyika kwenye Ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.
Mlimbwende
huyo, ambaye kabla ya kutwaa taji hilo alitawazwa kuwa Miss Temeke,
aliwabwaga warembo wengine 30 waliokuwa wakiwania taji hilo mwaka huu.
Kwa
ushindi huo, Siti amejinyakulia kitita cha Shilingi milioni 18, ambapo
ukumbini hapo alikabidhiwa hundi ya thamani ya Shilingi milioni 10 kwa
maelezo kwamba kiasi kilichobaki cha Shilingi milioni 8 atakabidhiwa
baada ya shindano hilo.
Siti
ataiwakilisha Tanzania kwenye shindano la Miss World mwakani, ambapo
mwaka huu Tanzania itawakilishwa na mshindi wa mwaka jana, Happiness
Watimanywa kutoka Dodoma.

No comments:
Post a Comment