Benki ya NBC tawi la Moshi.
Katika hukumu hiyo iliyotolewa jana na
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kilimanjaro, Simon
Kobelo, askofu huyo amehukumiwa kifungo hicho pamoja na raia watano wa
Kenya baada ya kupatikana na hatia ya kufanya wizi huo kwa mtutu wa
bunduki.
Moshi. Askofu wa Kanisa la Christian
Fellowship Assemblies of God la Arusha, Jumanne Kilongola amehukumiwa
kifungo cha miaka 32 jela baada ya kupatikana na hatia ya kupora Sh5.3
bilioni ndani ya Benki ya NBC, Tawi la Moshi Mei 21, 2004.
Katika hukumu hiyo iliyotolewa jana na
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kilimanjaro, Simon
Kobelo, askofu huyo amehukumiwa kifungo hicho pamoja na raia watano wa
Kenya baada ya kupatikana na hatia ya kufanya wizi huo kwa mtutu wa
bunduki.
Kati ya fedha hizo, Sh126.2 milioni
zilikuwa mali ya Benki ya NBC wakati Sh5.1 bilioni ni mali ya Benki Kuu
ya Tanzania (BoT) ambayo ilikuwa ikitumia NBC Moshi kama kituo chake
kidogo.
Ilielezwa mahakamani hapo wakati wa
ushahidi kuwa Askofu Kilongola ndiye aliyekodi gari aina ya Toyota
Landcruiser lililotumiwa kubeba fedha hizo kwa Sh320,000 na alimweleza
mmiliki wake kuwa alikuwa anakwenda kubeba wanakwaya wake.
Raia wa Kenya waliohukumiwa kifungo
hicho cha miaka 32 ni Wilfred Onyango Nganyi, Patrick Muthee Murithi,
Gabriel Kungu Kariuki, Jimmy Maina Njoroge na Simon Ndungu Kiambuthi.
Hata hivyo, mahakama hiyo iliwaachia
huru raia wengine watatu wa Kenya, Boniface Mwangi Mburu, David Ngugi
Mburu na Michael Mbanya Wathigo kutokana na kukosekana ushahidi dhidi
yao.
Hakimu Kobelo alisema upande wa mashtaka
ukiongozwa na mawakili wa Serikali, Hyra Sande, Ladslaus Komanya na
Stella Majaliwa umethibitisha pasipo shaka kuwa washtakiwa hao
waliohukumiwa walitenda makosa hayo.
Alisema ushahidi dhidi ya Askofu
Kilongola na raia hao wa Kenya ulikuwa madhubuti kutokana na kutambuliwa
kikamilifu na mashahidi katika gwaride la utambuzi.
Hakimu huyo alisema Mahakama imewahukumu
kifungo cha miaka 30 kwa unyang’anyi wa kutumia silaha na miaka mingine
miwili kwa kosa la kula njama ya kupora fedha hizo.
Hakimu Kobelo aliamuru Dola za Marekani
39,000, sawa na Sh64 milioni walizokutwa nazo washtakiwa zitaifishwe na
Serikali na zikabidhiwe kwa uongozi wa Benki ya NBC. Hukumu hiyo imekuja
wakati jitihada za Tanzania kuwarejesha nchini, wahalifu watatu kutoka
Kenya na Uganda, wanaodaiwa kuvamia benki hiyo zikiwa zimegonga mwamba.
Watuhumiwa hao ni Patrick Ayis Ingoi,
raia wa Kenya anayedaiwa kuwa kiongozi wa genge la majambazi hao,
Charles Lumago na Shaban Wayabona ambao ni raia wa Uganda.
Hukumu hiyo inafanya idadi ya
waliofungwa kwa uporaji huo kufikia 12, baada ya Watanzania wanne
kufungwa kwa kosa hilohilo Desemba 13, mwaka 2006.
chanzo; mwananchi.
chanzo; mwananchi.
No comments:
Post a Comment