
Aliyekuwa Mkurugenzi wa Shirika la Viwango Nchini (TBS), Charles Ekelege amehukumiwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kwenda jela miaka mitatu na kuilipa serikali Dola 42,543 za Kimarekani, baada ya kupatikana na hatia ya makosa matatu ikiwemo matumizi mabaya ya madaraka kwa kutoa asilimia 50.
Kadhalika, Ekelege anadaiwa kutoa asilimi hiyo ya punguzo la tozo ya utawala kwa Kampuni mbili Kampuni ya Jaffar Mohamed Ali Garage na Kampuni Quality Motors na kulisababishia shirika hilo hasara ya dola hizo.
Hukumu
hiyo imetolewa leo na Hakimu Mkazi Augustina Mmbando baada ya kupitia
ushahidi wa pande zote mbili na mahakama yake kumuona mshtakiwa bila
kuacha shaka ana hatia.
Hakimu
alisema ushahidi uliotolewa na upande wa Jamhuri ulieleza mahakama
kwamba mshtakiwa kupitia wadhifa wake alifanya maamuzi bila kinyume na
sheria za TBS zinazomwelekeza kuwasilisha masuala yote ya kiutendaji
kwenye Bodi ya Wakurugenzi.
Alisema
kitendo cha kutoa msamaha kwa kampuni hizo bila kuacha shaka moja kwa
moja mahakama imeona alitumia madaraka yake vibaya.
“Kwa
upande wa shitaka la pili, kiongozi yeyote katika Serikali ya Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania anapokuwa madarakani ni kwa ajili ya maslahi ya
taifa, lakini mshtakiwa alikosa uzalendo na kutumia madaraka yake vibaya
kuhujumu uchumi” alifafanua hakimu kuhusu ushahidi wa Jamhuri.
“Mahakama
inamuona mshtakiwa ana hatia katika kosa hili la pili la kujumu uchumi …
pia mshtakiwa amesababisha watanzania waliompa dhamana kukosa kula keki
ya taifa lao kwa kujinufaisha yeye binafsi” alisema hakimu huyo na
kuongeza kuwa.
“Katika
ushahidi uliotolewa na mshtakiwa alikiri kufanya maamuzi bila kupata
baraka na kibali cha Bodi ya Wakurugenzi na kwamba aliidanyanya
mahakama” alisema Hakimu Mmbando.
No comments:
Post a Comment