Friday, 11 July 2014

MAJANGA:BATULI SASA AKUBALI KUIGIZA NUSU UCHI


MWANADADA mkali wa Bongo Movies, Yobnesh Yusuph ‘Batuli’ amefunguka kuwa kwa sasa yupo tayari kuigiza nusu utupu kwa sinema za nje ya nchi.

Mwanadafada mkali wa Bongo Movies, Yobnesh Yusuph ‘Batuli’.
Akipiga stori mbili-tatu na kona hii, Batuli alisema kuwa muvi nyingi Bongo huwa zinafungiwa kwa kukosa maadili na kwamba kama ikitokea nafasi akaitwa nje ya nchi kuigiza sini hizo, atakuwa tayari.
“Zamani nilikuwa nikiogopa kuigiza nusu utupu. Wenzetu Nigeria wameendelea na ndiyo maana wanaigiza hata nusu utupu, kama itatokea nafasi ya kuigiza huko (nje ya Bongo) nusu utupu, nipo tayari,” alisema Batuli.

No comments:

Post a Comment