Friday, 6 June 2014

MTOTO ATEKETEA KWA MOTO NDANI.

MTOTO ATEKETEA KWA MOTO NDANI.


Mtoto mwenye umri wa miaka Mitatu na nusu aliyefahamika kwa jina la Rehema Patrick, amefariki dunia baada ya chumba alichokuwa amelala kuteketea kwa moto, hapo jana Mtaa wa Ilomba, jijini Mbeya.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kuongeza kuwa chanzo cha moto huo hakijafahamika ambapo mtoto huyo ambaye ni marehemu alikuwa amelala wakati mama yake mzazi aliyefahamika kwa jina la Winfrida Sokon (30), alikuwa ameenda kuchota maji huku naye baba yake akiwa safarini.

R.I.P Rehema

No comments:

Post a Comment