Saturday, 7 June 2014

Jini Kabula ayakana Mapenzi ya Baa....Asema kama unamtaka kimapenzi mfuate nyumbani



Jini Kabula ayakana Mapenzi ya Baa....Asema kama unamtaka kimapenzi mfuate nyumbani




Sitaki  tena....Ndivyo 
unavyoweza  kusema  kutokana  na kauli  ya  nyota  wa filamu  za 
kibongo  Mirium Jolwa  "Jini Kabula"  ambaye  amedai  kuwa  kwa  sasa 
hataki  kusikia  mapenzi  ya  pesa  na  kama  kuna  mwanaume 
anayemtaka  basi  amfuate  nyumbani  na  si  kuitana  baa.....


Kabula 
alisema  kuwa  wanaume  wengi  wamekuwa  na  tabia  ya  kuitana  baa 
huku  wakihisi  kuwa  kila  mwanamke  ni  mlevi  kutokana  na  tabia 
ya  baadhi  ya  wasanii  ambao  wamekuwa  wakijirahisisha  kwa  kupewa 
pombe...

"Siwezi  kuvua  nguo  eti  kwa  sababu  ya  pombe  wakati  hata  mwenyewe  naweza  kukaa  baa  na  kunywa  kwa  pesa  zangu. 

"Kama 
kuna  mwanaume  anataka  kutulia  na  mimi  si  lazima  tukae  baa 
kwani  kuna  sehemu  nzuri mnaweza  kukaa  na  kuzungumza, nasema  hivi 
ili  wale  wenye  tabia  hizo  waache  kabisa,"
alisema

No comments:

Post a Comment