WATUHUMIWA WA MLIPUKO WA MABOMU JIJINI ARUSHA WAPANDISHWA KIZIMBANI
Mmoja wa watuhumiwa hao akipakiwa kwenye Gari la Polisi tayari kwa Kupelekwa Mahakamani kusikiliza kesi yao.
WATU 17
wamepandishwa kizimbani katika mahakama ya hakimu Mkazi jijini Arusha,
kujibu mashitaka 16 yakiwemo ya kuua kwa kutumia bomu,kutesa binadamu na
kusajili vijana na kuwapeleka nje ya nchi kufanya ugaidi.
Watu hao
walifikishwa mahakamani hapo leo na kusomemewa shitaka hilo mbele ya
Hakimu Mkazi Mustafa Siama ambapo hawakutakiwa kujibu chochote kutokana
na kile kilichoelezwa kuwa mahakama hiyo haina uwezo wa kusikiliza kesi
hiyo.
CHANZO MTAA KWA MTAA



No comments:
Post a Comment