Thursday, 29 May 2014

KUMBUKUMBU YA MANGWEA WASANII KIBAO WAFURIKA KWENYE IBADA

KUMBUKUMBU YA MANGWEA WASANII KIBAO WAFURIKA KWENYE IBADA.

 Padri Octaviani Msimbe akiongoza ibada ya kumbukumbi ya kifo cha Albart Mangweha nyumbani kwao Kihonda 'Mazimbu Road' Morogoro
                         Padri Msimbe
 Padri Msimbe akisalimiana na mama mzazi wa Mangweha Bi Denisia Mangweha
 Mama Mangweha akipokea sakrameti takatifu

 Mchumba wa Mangweha  Michelle Louise raia ya Uingereza akihojiwa na Mtandao huu muda mfupi uliopita
 Msanii wa bongofleva Mgaza Pembe' M-2 THE- P ambaye alikuwa na m,arehemu Mangweha Afrika Kusini akipiga picha matukio ya lbada hiyo,
Mama Mangwea akitoa shukrani kwa watu walioshiriki lbada hiyo. 

Na Dustan Shekidele, Morogoro.
FAMILIA ya msanii nyota wa muziki wa Bongofleva marehemu Albert Keneth Mangweha aliyefariki ghafla  nchini Afrika Kusini May 28 mwaka jana, leo may 28 familia hiyo imefanya ibada nje ya viwanja vya nyumba yao iliyopo Kihonda 'Mazimbu Road' mkoani Morogoro,ya kumbukumbu ya mwaka mmoja wa kifo cha mpendwa wao huyo aliyekuwa na nyota ya kupendwa na  wengi.
Katika lbada hiyo iliyoongozwa na Paroko wa katika la Mtakatifu Monica Kihonda Padria Octaviani Msimbe ilihudhuliwa na wasanii kipa pamoja na mchumba wa marehmu Mangweha  Michelle Louise.

Kwa mujibu wa msemaji wa familia hiyo mama mzazi wa msanii huyo Bi,Denisia Mangweha, baada ya kukamilika kwa lbada hiyo leo jioni katika ukumbi wa Samaki Samaki Kihonda kutafanyia shughuri nyingine ya kumkumbuka msanii huyo.
" Pale Samaki samaki kutakuwa na shughuri mbili ya kwanza itaanza saa 12 jioni hadi saa mbili usiku na mafariki wa marehemu watafanya shughuri yao kuanza saa 2 usiku hadi majogoo hivyo tunawakaribisha wote mliofika kwenye ibada hii na mungu awabariki kwa kunikimbilia toka kifo cha mwanangu,mapaka hii leo sina cha kuwalipa mungu atawalipa asanteni sana"alisema mama huyo mwenye uso wa upole.

No comments:

Post a Comment